Visa vya wapenzi kuuana baada ya kurudiana vimekithiri nchini Kenya. Mara nyingi, mauaji hutokea baada ya mpenzi mmoja kushawishiwa na mwingine warudiane. Suala hili linatufanya kujiuliza je, ni sawa kurudiana na mtu uliyetengana naye? Aidha ni vigezo vipi ambavyo mtu anastahili kuzingatia kabla ya kurudiana na aliyekuwa mpenzi wake? Tumewashirikisha wananchi wanaotoa kauli zao vilevile kupata ushauri wa mtaalam wa masuala ya mapenzi.
view more