Siku hizi, mitandao ya kijamii imekuwa ikitumiwa na wengi kujitafutia wachumba, wengine wamefaulu na wengine wakikosa. Kijana mmoja amewasilisha malalamiko yake kupitia podcast hii akisema hamwamini tena mpenziwe wanayechumbiana mtandaoni akihisi kwamba anamchezea shere. Je, aendelee na uhusiano huo na mwanadada ambaye hajawahi kukutana naye ana kwa ana ama aukatize?
view more