Deliverance Church Zimmerman's Podcast
Religion & Spirituality:Christianity
Mweleze Yesu yanayokuhusu | Pst Zachary Muriithi | DCIKZ
Mariko 10:46-52
✊Wakafika Yeriko. Na Yesu alipokuwa akiondoka pamoja na Wanafunzi wake na umati wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando kando ya njia, akiomba. Aliposikia kuwa Yesu wa Nazareti alikuwa akipita, akaanza kupiga kelele, “Yesu, Mwana wa Daudi, nionee huruma!” Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya. Lakini yeye alipiga kelele zaidi, “Mwana wa Daudi, nionee huruma!” Yesu akasimama akawaambia, “Mwiteni.” Wakamwita wakamwambia, “Changamka! Usimame, anakuita.” Akatupa vazi lake kando, akaruka juu, akamwendea Yesu.
📌Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona tena.” Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Wakati huo huo akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.
✨Yesu alijua ya kuwa Bartimayo yuaja. Ila hakumuendea. Alipomwita alikuwa tayari kumsikiza.
✨Anataka umweleze yanayokuhusu.
#SundayService #Swahiliservice #mariko_10_46To52 #GreatCatch #dcikz #feelslikehome
Create your
podcast in
minutes
It is Free